0:00
0:00

Mlango 75

Ee Mungu, twakushukuru. Twakushukuru kwa kuwa Jina lako li karibu; Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu.
2 Nitakapoufikia wakati ulioamriwa, Mimi nitahukumu hukumu za haki.
3 Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki, Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake.
4 Naliwaambia waliojivuna, Msijivune; Na wasio haki, Msiiinue pembe.
5 Msiiinue pembe yenu juu, Wala msinene kwa shingo ya kiburi.
6 Maana siko mashariki wala magharibi, Wala nyikani itokako heshima.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye; Humdhili huyu na kumwinua huyu.
8 Maana mkononi mwa Bwana mna kikombe, Na mvinyo yake inatoka povu; Kumejaa machanganyiko; Naye huyamimina. Na sira zake wasio haki wa dunia Watazifyonza na kuzinywa.
9 Bali mimi nitatangaza matendo yako milele, Nitamwimbia Mungu wa Yakobo.
10 Pembe zote za wasio haki nitazikata, Na pembe za mwenye haki zitainuka.