0:00
0:00

Mlango 114

Haleluya. Israeli alipotoka Misri, Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni.
2 Yuda ilikuwa patakatifu pake, Israeli milki yake.
3 Bahari iliona ikakimbia, Yordani ilirudishwa nyuma.
4 Milima iliruka kama kondoo waume, Vilima kama wana-kondoo.
5 Ee bahari, una nini, ukimbie? Yordani, urudi nyuma?
6 Enyi milima, mruke kama kondoo waume? Enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana, Mbele za uso wa Mungu wa Yakobo.
8 Augeuza mwamba kuwa ziwa la maji, Jiwe gumu kuwa chemchemi.