0:00
0:00

Mlango 121

Nitayainua macho yangu niitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi?
2 Msaada wangu u katika Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.
3 Asiuache mguu wako usogezwe; Asisinzie akulindaye;
4 Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.
5 Bwana ndiye mlinzi wako; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.
6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.
7 Bwana atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.
8 Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.