0:00
0:00

Mlango 100

Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote;
2 Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba;
3 Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.
4 Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake;
5 Kwa kuwa Bwana ndiye mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake vizazi na vizazi.