0:00
0:00

Mlango 149

Haleluya. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Sifa zake katika kusanyiko la watauwa.
2 Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya, Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa matari na kinubi wamwimbie.
4 Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake, Huwapamba wenye upole kwa wokovu.
5 Watauwa na waushangilie utukufu, Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao.
6 Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao, Na upanga mkali kuwili mikononi mwao.
7 Ili kufanya kisasi juu ya mataifa, Na adhabu juu ya kabila za watu.
8 Wawafunge wafalme wao kwa minyororo, Na wakuu wao kwa pingu za chuma.
9 Kuwafanyia hukumu iliyoandikwa; Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote. Haleluya.