0:00
0:00

Mlango 122

Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa Bwana.
2 Miguu yetu imesimama Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.
3 Ee Yerusalemu uliyejengwa Kama mji ulioshikamana,
4 Huko ndiko walikopanda kabila, Kabila za Bwana; Ushuhuda kwa Israeli, Walishukuru jina la Bwana.
5 Maana huko viliwekwa viti vya hukumu, Viti vya enzi vya mbari ya Daudi.
6 Utakieni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao;
7 Amani na ikae ndani ya kuta zako, Na kufanikiwa ndani ya majumba yako.
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu Niseme sasa, Amani ikae nawe.
9 Kwa ajili ya nyumba ya Bwana, Mungu wetu, Nikutafutie mema.