0:00
0:00

Mlango 67

Mungu na atufadhili na kutubariki, Na kutuangazia uso wake.
2 Njia yake ijulike duniani, Wokovu wake katikati ya mataifa yote.
3 Watu na wakushukuru, Ee Mungu, Watu wote na wakushukuru.
4 Mataifa na washangilie, Naam, waimbe kwa furaha, Maana kwa haki utawahukumu watu, Na kuwaongoza mataifa walioko duniani.
5 Watu na wakushukuru, Ee Mungu, Watu wote na wakushukuru.
6 Nchi imetoa mazao yake MUNGU, Mungu wetu, ametubariki.
7 Mungu atatubariki sisi; Miisho yote ya dunia itamcha Yeye.