0:00
0:00

Mlango 130

Ee Bwana, toka vilindini nimekulilia.
2 Bwana, uisikie sauti yangu. Masikio yako na yaisikilize Sauti ya dua zangu.
3 Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?
4 Lakini kwako kuna msamaha, Ili Wewe uogopwe.
5 Nimemngoja Bwana, roho yangu imengoja, Na neno lake nimelitumainia.
6 Nafsi yangu inamngoja Bwana, Kuliko walinzi waingojavyo asubuhi, Naam, walinzi waingojao asubuhi.
7 Ee Israeli, umtarajie Bwana; Maana kwa Bwana kuna fadhili, Na kwake kuna ukombozi mwingi.
8 Yeye atamkomboa Israeli na maovu yake yote.