0:00
0:00

Mlango 123

Nimekuinulia macho yangu, Wewe uketiye mbinguni.
2 Kama vile macho ya watumishi Kwa mkono wa bwana zao Kama macho ya mjakazi Kwa mkono wa bibi yake; Hivyo macho yetu humwelekea Bwana, Mungu wetu, Hata atakapoturehemu.
3 Uturehemu, Ee Bwana, uturehemu sisi, Kwa maana tumeshiba dharau.
4 Nafsi zetu zimeshiba mzaha wa wenye raha, Na dharau ya wenye kiburi.