0:00
0:00

Mlango 120

Katika shida yangu nalimlilia Bwana Naye akaniitikia.
2 Ee Bwana, uiponye nafsi yangu Na midomo ya uongo na ulimi wa hila.
3 Akupe nini, akuzidishie nini, Ewe ulimi wenye hila?
4 Mishale ya mtu hodari iliyochongoka, Pamoja na makaa ya mretemu.
5 Ole wangu mimi! Kwa kuwa nimekaa katika Mesheki; Na kufanya maskani yangu Katikati ya hema za Kedari.
6 Nafsi yangu imekaa siku nyingi, Pamoja naye aichukiaye amani.
7 Mimi ni wa amani; Bali ninenapo, wao huelekea vita.