0:00
0:00

Mlango 20

Bwana akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.
2 Akupelekee msaada toka patakatifu pake, Na kukutegemeza toka Sayuni.
3 Azikumbuke sadaka zako zote, Na kuzitakabali dhabihu zako.
4 Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kuyatimiza mashauri yako yote.
5 Na tuushangilie wokovu wako, Kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu. Bwana akutimizie matakwa yako yote.
6 Sasa najua kuwa Bwana amwokoa masihi wake;Atamjibu kutoka mbingu zake takatifu.
7 Hawa wanataja magari na hawa farasi, Bali sisi tutalitaja jina la Bwana, Mungu wetu.
8 Wao wameinama na kuanguka, Bali sisi tumeinuka na kusimama.
9 Bwana, umwokoe mfalme, Utuitikie siku tuitayo.