0:00
0:00

Mlango 126

Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni, Tulikuwa kama waotao ndoto.
2 Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko, Na ulimi wetu kelele za furaha. Ndipo waliposema katika mataifa, Bwana amewatendea mambo makuu.
3 Bwana alitutendea mambo makuu, Tulikuwa tukifurahi.
4 Ee Bwana, uwarejeze watu wetu waliofungwa, Kama vijito vya Kusini.
5 Wapandao kwa machozi Watavuna kwa kelele za furaha.
6 Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.