0:00
0:00

Mlango 128

Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake.
2 Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema.
3 Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, Vyumbani mwa nyumba yako. Wanao kama miche ya mizeituni Wakiizunguka meza yako.
4 Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye Bwana.
5 Bwana akubariki toka Sayuni; Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;
6 Naam, ukawaone wana wa wanao. Amani ikae na Israeli.