0:00
0:00

Mlango 6

Wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.
2 Na wana wa Kohathi; Amramu, na Ishari, na Hebroni, na Uzieli.
3 Na wana wa Amramu; Haruni, na Musa, na Miriamu. Na wana wa Haruni; Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari.
4 Eleazari akamzaa Finehasi; na Finehasi akamzaa Abishua;
5 na Abishua akamzaa Buki; na Buki akamzaa Uzi;
6 na Uzi akamzaa Zerahia; na Zerahia akamzaa Merayothi,
7 na Merayothi akamzaa Amaria; na Amaria akamzaa Ahitubu;
8 na Ahitubu akamzaa Sadoki; na Sadoki akamzaa Ahimaasi;
9 na Ahimaasi akamzaa Azaria; na Azaria akamzaa Yohana;
10 na Yohana akamzaa Azaria (ndiye huyo aliyefanya kazi ya ukuhani katika nyumba aliyoijenga Sulemani huko Yerusalemu)
11 na Azaria akamzaa Amaria; na Amaria akamzaa Ahitubu;
12 na Ahitubu akamzaa Sadoki; na Sadoki akamzaa Meshulamu;
13 na Meshulamu akamzaa Hilkia; na Hilkia akamzaa Azaria;
14 na Azaria akamzaa Seraya; na Seraya akamzaa Yehosadaki;
15 na Yehosadaki akachukuliwa mateka, hapo Bwana alipowachukua mateka Yuda na Yerusalemu, kwa mkono wa Nebukadreza.
16 Wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.
17 Na haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni; Libni, na Shimei.
18 Na wana wa Kohathi walikuwa Amramu, na Ishari, na Hebroni, na Uzieli.
19 Wana wa Merari; Mali, na Mushi. Na hizi ndizo jamaa za Walawi, sawasawa na mbari za baba zao.
20 Wa Gershoni; mwanawe huyo ni Libni, na mwanawe huyo ni Yahathi, na mwanawe huyo ni Zima;
21 na mwanawe huyo ni Yoa, na mwanawe huyo ni Ido, na mwanawe huyo ni Zera, na mwanawe huyo ni Yeatherai.
22 Wana wa Kohathi; mwanawe huyo ni Ishari, na mwanawe huyo ni Kora, na mwanawe huyo ni Asiri;
23 na mwanawe huyo ni Elkana, na mwanawe huyo ni Ebiasafu, na mwanawe huyo ni Asiri;
24 na mwanawe huyo ni Tahathi, na mwanawe huyo ni Urieli, na mwanawe huyo ni Uzia, na mwanawe huyo ni Shauli.
25 Na wana wa Elkana; Amasai, na Ahimothi.
26 Kwa habari za Elkana; wana wa Elkana; mwanawe huyo ni Sufu, na mwanawe huyo ni Tohu;
27 na mwanawe huyo ni Elihu, na mwanawe huyo ni Yerohamu, na mwanawe huyo ni Elkana.
28 Na wana wa Samweli; Yoeli, mzaliwa wa kwanza, na wa pili Abia.
29 Wana wa Merari; Mali, na mwanawe huyo ni Libni, na mwanawe huyo ni Shimei, na mwanawe huyo ni Uza;
30 na mwanawe huyo ni Shimea, na mwanawe huyo ni Hagla, na mwanawe huyo ni Asaya.
31 Na hawa ndio watu aliowaweka Daudi juu ya kazi ya kuimba katika nyumba ya Bwana, sanduku lile lilipokwisha pata mahali pa kustarehe.
32 Nao wakafanya kazi yao ya kuimba mbele ya maskani ya hema ya kukutania, hata Sulemani alipokuwa amejenga ile nyumba ya Bwana huko Yerusalemu; pia wakaisimamia huduma yao sawasawa na zamu zao.
33 Na hawa ndio waliofanya huduma pamoja na wana wao. Katika wana wa Wakohathi; Hemani mwimbaji, mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli;
34 mwana wa Elkana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu, mwana wa Tohu;
35 mwana wa Sufu, mwana wa Elkana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai;
36 mwana wa Elkana, mwana wa Shauli, mwana wa Uzia, mwana wa Urieli;
37 mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora;
38 mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli.
39 Na nduguye Asafu, aliyesimama upande wake wa kuume, huyo Asafu alikuwa mwana wa Berekia, mwana wa Shimea;
40 mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya;
41 mwana wa Yeatherai, mwana wa Zera, mwana wa Ido;
42 mwana wa Yoa, mwana wa Zima, mwana wa Shimei;
43 mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
44 Na upande wa kushoto ndugu zao, wana wa Merari; Ethani, mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki;
45 mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia;
46 mwana wa Amzi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri;
47 mwana wa Mali, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
48 Na ndugu zao, Walawi, ndio waliowekwa ili kufanya huduma yote ya maskani ya nyumba ya Mungu.
49 Lakini Haruni na wanawe ndio waliokuwa wakitoa sadaka juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na juu ya madhabahu ya kufukizia uvumba, kwa ajili ya kazi yote ya Patakatifu pa Patakatifu, ili kufanya upatanisho kwa Israeli, sawasawa na yote aliyokuwa ameyaamuru Musa, mtumishi wa Mungu.
50 Na hawa ndio wana wa Haruni; mwanawe huyo ni Eleazari, na mwanawe huyo ni Finehasi, na mwanawe huyo ni Abishua;
51 na mwanawe huyo ni Buki, na mwanawe huyo ni Uzi, na mwanawe huyo ni Serahia;
52 na mwanawe huyo ni Merayothi, na mwanawe huyo ni Amaria, na mwanawe huyo Ahitubu;
53 na mwanawe huyo ni Sadoki, na mwanawe huyo ni Ahimaasi.
54 Basi haya ndiyo makao yao, sawasawa na marago yao mipakani mwao; wana wa Haruni, katika jamaa za Wakohathi; kwani walikuwa na kura ya kwanza;
55 wakapewa Hebroni, katika nchi ya Yuda, na vijiji vyake vilivyouzunguka;
56 bali mashamba ya mji huo, na vijiji vyake, alipewa Kalebu, mwana wa Yefune.
57 Na wana wa Haruni wakapewa miji ile ya kukimbilia, nayo ni Hebroni, tena Libna pamoja na viunga vyake, na Yatiri, na Eshtemoa pamoja na viunga vyake;
58 na Holoni pamoja na viunga vyake, na Debiri pamoja na viunga vyake;
59 na Ashani pamoja na viunga vyake, na Beth-shemeshi pamoja na viunga vyake;
60 tena katika kabila ya Benyamini; Geba pamoja na viunga vyake, na Alemethi pamoja na viunga vyake, na Anathothi pamoja na viunga vyake. Miji yao yote katika jamaa zao ilikuwa miji kumi na mitatu.
61 Nao waliobaki wa wana wa Kohathi walipewa kwa kura miji kumi, katika jamaa ya kabila hiyo, yaani, nusu-kabila, nusu ya Manase.
62 Na wana wa Gershoni walipewa kwa kura miji kumi na mitatu, sawasawa na jamaa zao, katika kabila ya Isakari, na katika kabila ya Asheri, na katika kabila ya Naftali, na katika kabila ya Manase waliokaa Bashani.
63 Na wana wa Merari walipewa kwa kura miji kumi na miwili, sawasawa na jamaa zao, katika kabila ya Reubeni, na katika kabila ya Gadi, na katika kabila ya Zabuloni.
64 Na wana wa Israeli waliwapa Walawi miji hiyo pamoja na viunga vyake.
65 Tena wakawapa kwa kura miji hiyo iliyotajwa majina yake, katika kabila ya wana wa Yuda, na katika kabila ya wana wa Simeoni, na katika kabila ya wana wa Benyamini.
66 Na jamaa nyingine za wana wa Kohathi walikuwa na miji ya mipakani mwao katika kabila ya Efraimu.
67 Basi wakapewa miji ya kukimbilia, yaani, Shekemu pamoja na viunga vyake katika nchi ya milima milima ya Efraimu; na Gezeri pamoja na viunga vyake;
68 na Yokmeamu pamoja na viunga vyake, na Beth-horoni pamoja na viunga vyake;
69 na Aiyaloni pamoja na viunga vyake, na Gath-rimoni pamoja na viunga vyake;
70 na katika nusu-kabila ya Manase; Taanaki pamoja na viunga vyake, na Ibleamu pamoja na viunga vyake; kwa mabaki ya jamaa ya wana wa Kohathi.
71 Na wana wa Gershoni wakapewa, katika jamaa ya nusu-kabila ya Manase; Golani katika Bashani pamoja na viunga vyake, na Ashtarothi pamoja na viunga vyake;
72 na katika kabila ya Isakari; Kishioni pamoja na viunga vyake, na Daberathi pamoja na viunga vyake;
73 na Remethi pamoja na viunga vyake, na En-gaminu pamoja na viunga vyake;
74 na katika kabila ya Asheri; Mishali pamoja na viunga vyake, na Abdoni pamoja na viunga vyake;
75 na Helkathi pamoja na viunga vyake, na Rehobu pamoja na viunga vyake;
76 na katika kabila ya Naftali; Kedeshi katika Galilaya pamoja na viunga vyake, na Hamothi pamoja na viunga vyake, na Kiriathaimu pamoja na viunga vyake.
77 Nao mabaki ya Walawi, wana wa Merari, wakapewa, katika kabila ya Zabuloni; Rimona pamoja na viunga vyake, na Tabori pamoja na viunga vyake;
78 na ng'ambo ya mto wa Yordani huko Yeriko, upande wa mashariki wa Yordani, katika kabila ya Reubeni; Bezeri katika nyika pamoja na viunga vyake, na Yahasa pamoja na viunga vyake,
79 na Kedemothi pamoja na viunga vyake, na Mefaathi pamoja na viunga vyake;
80 na katika kabila ya Gadi; Ramothi katika Gileadi pamoja na viunga vyake, na Mahanaimu pamoja na viunga vyake;
81 na Heshboni pamoja na viunga vyake, na Yazeri pamoja na viunga vyake.