0:00
0:00

Mlango 12

Basi hawa ndio wafalme wa nchi, ambao wana wa Israeli waliwapiga na kuimiliki nchi yao ng'ambo ya pili ya Yordani, upande wa maawio ya jua, kutoka bonde la Amoni mpaka mlima wa Hermoni, na nchi yote ya Araba upande wa mashariki;
2 Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekaa huko Heshboni, naye ndiye aliyetawala toka Aroeri, ulioko kando ya bonde la Arnoni, na toka huo mji ulio katikati ya bonde, na nusu ya Gileadi, hata kuufikilia mto wa Yaboki, mpaka wa hao wana wa Amoni;
3 na nchi ya Araba mpaka bahari ya Kinerethi, kuelekea mashariki, tena mpaka bahari ya Ataba, mpaka Bahari ya Chumvi, kwendea mashariki, njia ya kwendea Beth-yeshimothi; tena upande wa kusini, chini ya matelemko ya Pisga;
4 tena mpaka wa Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa wa hayo mabaki ya hao Warefai, aliyekaa Ashtarothi na Edrei,
5 naye alitawala katika mlima wa Hermoni, na katika Saleka, na katika Bashani yote, hata mpaka wa Wageshuri, na Wamaaka, na nusu ya Gileadi, mpaka wa huyo Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Musa mtumishi wa Bwana na wana wa Israeli wakawapiga; naye Musa mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, na Wagadi, na nusu ya kabila ya Manase iwe urithi wao.
7 Hawa ni wafalme wa hiyo nchi ambao Yoshua na wana wa Israeli waliwapiga ng'ambo ya pili ya Yordani upande wa magharibi, kutoka Baal-gadi katika bonde la Lebanoni mpaka kilima cha Halaki, kilichoelekea Seiri; Yoshua naye akawapa kabila za Israeli iwe milki yao sawasawa na magawanyo yao;
8 katika nchi ya vilima, na katika Shefela, na katika nchi ya Araba, na katika matelemko, na katika bara, na katika Negebu; nchi ya Mhiti, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi;
9 mfalme wa Yeriko, mmoja; mfalme wa Ai, ulio karibu na Betheli, mmoja;
10 mfalme wa Yerusalemu, mmoja; mfalme wa Hebroni, mmoja;
11 mfalme wa Yarmuthi, mmoja; na mfalme wa Lakishi, mmoja;
12 mfalme wa Egloni, mmoja; na mfalme wa Gezeri, mmoja;
13 mfalme wa Debiri, mmoja; na mfalme wa Gederi, mmoja;
14 mfalme wa Horma, mmoja; na mfalme wa Aradi, mmoja;
15 mfalme wa Libna, mmoja; na mfalme wa Adulamu, mmoja;
16 mfalme wa Makeda, mmoja; na mfalme wa Betheli, mmoja;
17 mfalme wa Tapua, mmoja; na mfalme wa Heferi, mmoja;
18 mfalme wa Afeka, mmoja; na mfalme wa Lasharoni, mmoja;
19 mfalme wa Madoni, mmoja; na mfalme wa Hazori, mmoja;
20 mfalme wa Shimron-meroni, mmoja; na mfalme wa Akshafu, mmoja;
21 mfalme wa Taanaki, mmoja; na mfalme wa Megido, mmoja;
22 na mfalme wa Kedeshi, mmoja; mfalme wa Yokneamu wa Karmeli, mmoja;
23 mfalme wa Dori katika kilima cha Dori, mmoja; na mfalme wa makabila katika Gilgali, mmoja;
24 na mfalme wa Tirsa, mmoja; wafalme hao wote walikuwa ni thelathini na mmoja.