Kupumzika na likizo

0:00
0:00

  • Nalijilaza nikalala usingizi, nikaamka, Kwa kuwa Bwana ananitegemeza.
    Zaburi 3:5
  • Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama.
    Zaburi 4:8
  • Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,
    Zaburi 91:5
  • Yeye humpa mpenzi wake usingizi.
    Zaburi 127:2
  • Ulalapo hutaona hofu; Naam, utalala na usingizi wako utakuwa mtamu.
    Mithali 3:24
  • Usingizi wake kibarua ni mtamu, kwamba amekula kidogo, au kwamba amekula kingi; lakini kushiba kwake tajiri hakumwachi kulala usingizi.
    Mhubiri 5:12
  • Yeye huingia katika amani; wao hustarehe katika vitanda vyao, kila mtu aendaye katika unyofu wake.
    Isaya 57:2
  • Na ahimidiwe Bwana, aliyewapa watu wake Israeli kustarehe, vile vile kama yote aliyoyaahidi. Halikukosa kupatikana neno lo lote katika ahadi yake njema, aliyoahidi kwa mkono wa Musa, mtumishi wake.
    1 Wafalme 8:56
  • Nawe utakuwa salama, kwa sababu kuna matumaini; Naam, utatafuta-tafuta kando yako, na kupumzika katika salama.
    Ayubu 11:18
  • Yeye huingia katika amani; wao hustarehe katika vitanda vyao, kila mtu aendaye katika unyofu wake.
    Isaya 57:2
  • Kama ukigeuza mguu wako usihalifu sabato, usifanye anasa yako siku ya utakatifu wangu; ukiita sabato siku ya furaha, na siku takatifu ya Bwana yenye heshima; ukiitukuza, kwa kutokuzifanya njia zako mwenyewe, wala kuyatafuta yakupendezayo, wala kusema maneno yako mwenyewe; ndipo utakapojifurahisha katika Bwana; nami nitakupandisha mahali pa nchi palipoinuka; nitakulisha urithi wa Yakobo baba yako; kwa maana kinywa cha Bwana kimenena hayo.
    Isaya 58:13, 14
  • Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
    1 Wakorintho 10:31
  • Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu. Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake.
    Waebrania 4:9, 10