Mstari wa Siku

[Copy and send, from here:]

Mstari wa Siku:

Habari za asubuhi! 🙂

https://www.wordproject.org/bibles/votd/index_sw.htm


Mistari ya kila mwezi ya Biblia:

Nov. 1
"Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?"
- Warumi 8:35

Nov. 2
" Basi msihukumu hukumu ya macho tu, bali ifanyeni hukumu iliyo ya haki."
- Yohana 7:24

Nov. 3
"Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele."
- Zaburi 73:26

Nov. 4
"Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi."
- 1 Petro 4:8

Nov. 5
"Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko."
- Mithali 16:18

Nov. 6
"Mimi naiumba nuru, na kulihuluku giza; mimi nafanya suluhu, na kuhuluku ubaya; Mimi ni Bwana, niyatendaye hayo yote."
- Isaya 45:7

Nov. 7
"shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu."
- 1 Wathesalonike 5:18

Nov. 8
"Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze."
- 1 Petro 5:8

Nov. 9
"na masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto."
- Isaya 30:21

Nov. 10
"Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake."
- Waebrania 13:15

Nov. 11
"Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali."
- Mithali 22:15

Nov. 12
"Nitasema, Bwana ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini."
- Zaburi 91:2

Nov. 13
"Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo."
- Wafilipi 4:11

Nov. 14
"Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu."
- Mathayo 5:9

Nov. 15
"Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu."
- 1 Wakorintho 10:31

Nov. 16
"Kwa maana Bwana MUNGU, Mtakatifu wa Israeli, asema hivi, Kwa kurudi na kustarehe mtaokolewa; nguvu zenu zitakuwa katika kutulia na kutumaini; lakini hamkukubali."
- Isaya 30:15

Nov. 17
"Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. -"
- Ufunuo wa Yohana 3:20

Nov. 18
"Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima."
- Warumi 13:7

Nov. 19
"tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu."
- Waebrania 12:2

Nov. 20
"Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana."
- 1 Yohana 4:11

Nov. 21
"Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu."
- Wafilipi 4:7

Nov. 22
"Hatua za mtu zaimarishwa na Bwana, Naye aipenda njia yake."
- Zaburi 37:23

Nov. 23
"Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea."
- Mathayo 21:22

Nov. 24
"mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi."
- Colossians 3:13

Nov. 25
"Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili."
- 1 Wakorintho 10:13

Nov. 26
"Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa."
- Luke 6:38

Nov. 27
"Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii."
- James 5:16

Nov. 28
"Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama."
- Mithali 18:10

Nov. 29
"Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa."
- Waebrania 13:5

Nov. 30
" Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu."
- Warumi 8:18