Mstari wa Siku

[Copy and send, from here:]

Mstari wa Siku:

Habari za asubuhi! 🙂

https://www.wordproject.org/bibles/votd/index_sw.htm


Mistari ya kila mwezi ya Biblia:


Siku 1
"Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini Bwana humponya nayo yote.
- Zaburi 34:19


Siku 2
"Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.
- Yohana 15:7

Siku 3
"Kwa kuwa Bwana ampenSikue humrudi, Kama vile baba mwanawe ampendezaye.
- Mithali 3:12

Siku 4
"Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu.
- Yohana 16:24

Siku 5
"Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.
- 1 Yohana 1:9

Siku 6
"...na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.
- Mathayo 16:18

Siku 7
"Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako ziko furaha tele; Na katika mkono wako wa kuume Mna mema ya milele.
- Zaburi 16:11

Siku 8
"...Uwe hodari, mwenye moyo mkuu, ukatende hivyo; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu, Mungu wangu, yu pamoja nawe; ...
- 1 Mambo ya Nyakati 28:20

Siku 9
"Mungu akaumba nyangumi wakubwa, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, ...Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
- Mwanzo 1:21

Siku 10
"Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Kwa maana ametenda mambo ya ajabu. Mkono wa kuume wake mwenyewe, Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu.
- Zaburi 98:1

Siku 11
"Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.
- Mithali 28:13

Siku 12
"zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
- Waefeso 6:16

Siku 13
"Utabarikiwa kuliko mataifa yote; hakutakuwa na mtu mume wala mke aliye tasa kati yenu; ...
- Kumbukumbu la Torati 7:14

Siku 14
"Kumcha Bwana ni tumaini imara; Watoto wake watakuwa na kimbilio.
- Mithali 14:26

Siku 15
"If it be possible, as much as lieth in you, live peaceably with all men.
- Warumi 12:18

Siku 16
"Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama.
- Zaburi 4:8

Siku 17
" Naye Bwana, yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike.
- Kumbukumbu la Torati 31:8

Siku 18
"Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.
- Yohana 8:36

Siku 19
"...Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. ...
- Luka 23:34

Siku 20
"...Paza sauti kwa nguvu; Paza sauti yako, usiogope; Iambie miji ya Yuda, Tazameni, Mungu wenu.
- Isaya 40:9

Siku 21
"...Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;
- Yohana 11:25

Siku 22
"Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu; Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.
- Mithali 11:2

Siku 23
"Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
- Zaburi 23:4

Siku 24
"Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki.
- Yakobo 3:17

Siku 25
"mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.
- Waefeso 4:24

Siku 26
"...na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.
- Mathayo 16:19

Siku 27
"Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.
- Kutoka 23:20

Siku 28
"And said, For this cause shall a man leave father and mother, and shall cleave to his wife: and they twain shall be one flesh?
- Mathayo 19:5

Siku 29
"akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
- 1 Wakorintho 2:4

Siku 30
"Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. -
- Yohana 3:16