Mstari wa Siku

Habari za asubuhi! 🙂


Mistari ya kila mwezi ya Biblia:


Februari 1
"Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu.
- Yohana 12:32


Februari 2
"Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.
- Mithali 20:1

Februari 3
"Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo; Majivuno yasitoke vinywani mwenu; Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa maarifa, Na matendo hupimwa na yeye kwa mizani.
- 1 Samweli 2:3

Februari 4
"Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.
- Isaya 65:24

Februari 5
"Mataifa yote huwa kama si kitu mbele zake; huhesabiwa kwake kuwa duni ya si kitu, na ubatili.
- Isaya 40:17

Februari 6
"Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.
- Mambo ya Walawi 20:13

Februari 7
"Basi, wataliogopa jina la Bwana toka magharibi, na utukufu wake toka maawio ya jua; maana yeye atakuja kama mkondo wa mto ufurikao, uendeshwao kwa pumzi ya Bwana.
- Isaya 59:19

Februari 8
"Ondoka, ukatembee katika nchi hii katika mapana yake, na marefu yake, maana nitakupa wewe nchi hiyo.
- Mwanzo 13:17

Februari 9
"Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
- Mwanzo 2:24

Februari 10
" Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; -
- Yohana 1:12

Februari 11
"Bwana, asubuhi utaisikia sauti yangu, Asubuhi nitakupangia dua yangu na kutazamia.
- Zaburi 5:3

Februari 12
"kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.
- Nehemiah 8:10

Februari 13
"Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.
- Mithali 3:5,6

Februari 14
"Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
- Mathayo 22:37

Februari 15
"bali wewe simama hapa sasa, ili nikuambie neno la Mungu.
- 1 Samweli 9:27

Februari 16
"Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, Na kumfahamisha mjinga.
- Zaburi 119:130

Februari 17
"Nalimtafuta Bwana akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote.
- Zaburi 34:4

Februari 18
"Wana-simba hutindikiwa, huona njaa; Bali wamtafutao Bwana hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema.
- Zaburi 34:10

Februari 19
"Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili; Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;
- Zaburi 18:25

Februari 20
"Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumaini Bwana
- Zaburi 40:3

Februari 21
"Mheshimu Bwana kwa mali yako, Na kwa malimbuko ya mazao yako yote. Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.
- Mithali 3:9,10

Februari 22
"Bwana, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya;
- 2 Wafalme 20:5

Februari 23
"Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.
- Warumi 10:17

Februari 24
"Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
- Waebrania 11:1

Februari 25
"Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini, bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu; huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.
- Warumi 4:20, 21

Februari 26
"Nao wote wanaokukimbilia watafurahi; Watapiga daima kelele za furaha. Kwa kuwa Wewe unawahifadhi, Walipendao jina lako watakufurahia.
- Zaburi 5:11

Februari 27
"Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.
- James 4:8

Februari 28
"na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake.
- 1 Yohana 3:22