Hekima na maamuzi

0:00
0:00

  • akawaambia hao makadhi, Angalieni myafanyayo; kwa kuwa hammfanyii mwanadamu hukumu, ila Bwana; naye yupo pamoja nanyi katika neno la hukumu.
    2 Mambo ya Nyakati 19:6
  • Naam, ukiita busara, Na kupaza sauti yako upate ufahamu; Ndipo utakapofahamu kumcha Bwana, Na kupata kumjua Mungu. Kwa kuwa Bwana huwapa watu hekima; Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu;
    Mithali 2:3, 5, 6
  • Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana.
    Mithali 16:1
  • Watu wabaya hawaelewi na hukumu; Bali wamtafutao Bwana huelewa na yote.
    Mithali 28:5
  • Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana; na furaha yake itakuwa katika kumcha Bwana; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa masikio yake;
    Isaya 11:2, 3
  • Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima; Danieliii naye alikuwa na ufahamu katika maono yote, na ndoto.
    Danieli 1:17
  • Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.
    Yakobo 1:5
  • Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi, Kwa maana nimekutumaini Wewe. Unijulishe njia nitakayoiendea, Kwa maana nakuinulia nafsi yangu.
    Zaburi 143:8
  • Unifundishe kuyatenda mapenzi yako, Kwa maana ndiwe Mungu wangu; Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa, Ee Bwana, unihuishe kwa ajili ya jina lako, Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni;
    Zaburi 143:10, 11
  • mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.
    Mithali 1:5
  • Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
    Mithali 12:15
  • Pasipo mashauri makusudi hubatilika; Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.
    Mithali 15:22
  • Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.
    Mithali 19:20
  • Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana; Na kwa shauri la akili fanya vita.
    Mithali 20:18
  • Maana kwa mashauri ya akili utafanya vita; Na kwa wingi wa washauri huja wokovu.
    Mithali 24:6
  • Basi msihukumu hukumu ya macho tu, bali ifanyeni hukumu iliyo ya haki.
    Yohana 7:24
  • Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki.
    Yakobo 3:17
  • Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa.
    2 Wakorintho 13:1