Mimba na uzazi

0:00
0:00

  • Naam, kwa Mungu wa baba yako atakaye kusaidia; Kwa mibaraka ya mbinguni juu. Mibaraka ya vilindi vilivyo chini, Mibaraka ya maziwa, na ya mimba.
    Mwanzo 49:25
  • Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao.
    Kutoka 1:7
  • naye atakupenda na kukubarikia na kukuongeza tena ataubarikia uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, nafaka zako na divai yako, na mafuta yako, maongeo ya ng'ombe zako, na wadogo wa kondoo zako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwa atakupa. Utabarikiwa kuliko mataifa yote; hakutakuwa na mtu mume wala mke aliye tasa kati yenu; wala kati ya wanyama wenu wa mifugo.
    Kumbukumbu la Torati 7:13, 14
  • Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye? Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni?
    Ayubu 31:15
  • Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.
    Zaburi 112:2
  • Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, Awe mama ya watoto mwenye furaha.
    Zaburi 113:9
  • Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu.
    Zaburi 127:3
  • Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, Uliniunga tumboni mwa mama yangu.
    Zaburi 139:13
  • Maana ameyakaza mapingo ya malango yako, Amewabariki wanao ndani yako.
    Zaburi 147:13
  • Atalilisha kundi lake kama mchungaji, Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake; Na kuwachukua kifuani mwake, Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole.
    Isaya 40:11
  • Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa; nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji.
    Isaya 44:3, 4
  • Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
    Yeremia 1:5
  • Naye heri aliyesadiki; kwa maana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana.
    Luka 1:45
  • Kwa imani hata Sara mwenyewe alipokea uwezo wa kuwa na mimba; alipokuwa amepita wakati wake; kwa kuwa alimhesabu yeye aliyeahidi kuwa mwaminifu.
    Waebrania 11:11
  • Akanitoa akanipeleka panapo nafasi, Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.
    Zaburi 18:19
  • Unitegee sikio lako, uniokoe hima. Uwe kwangu mwamba wa nguvu, Nyumba yenye maboma ya kuniokoa.
    Zaburi 31:2
  • Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
    Zaburi 34:7
  • Ee Bwana, uwe radhi kuniokoa, Ee Bwana, unisaidie hima.
    Zaburi 40:13
  • Nami ni maskini na mhitaji, Bwana atanitunza. Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, Ee Mungu wangu, usikawie.
    Zaburi 40:17
  • Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.
    Zaburi 50:15
  • Toka mwisho wa nchi nitakulilia nikizimia moyo, Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda.
    Zaburi 61:2
  • Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.
    Zaburi 91:14
  • Bali wazao wa wenye haki wataokoka.
    Mithali 11:21
  • Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka; bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
    Isaya 40:29-31
  • Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na Bwana, na watoto wao pamoja nao.
    Isaya 65:23
  • Kabla hajaona utungu alizaa; Kabla maumivu yake hayajampata, Alizaa mtoto mwanamume. Je! Mimi nilete wana karibu na kuzaliwa, nisizalishe? Asema Bwana; mimi nizalishaye, je! Nilifunge tumbo? Asema Mungu wako.
    Isaya 66:7, 9
  • Mwanamke azaapo, yuna huzuni kwa kuwa saa yake imefika; lakini akiisha kuzaa mwana, haikumbuki tena ile dhiki, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtu ulimwenguni.
    Yohana 16:21
  • Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.
    1 Wakorintho 10:13
  • Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
    2 Wakorintho 12:9
  • Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.
    Wagalatia 6:9
  • Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
    Wafilipi 4:13
  • Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi.
    1 Timotheo 2:15