Uaminifu

0:00
0:00

  • Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake;
    Wakolosai 3:9
  • Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.
    Warumi 12:17
  • tukitangulia kufikiri yaliyo mema, si mbele za Bwana tu, ila na mbele ya wanadamu.
    2 Wakorintho 8:21
  • Mizani ya hadaa ni chukizo kwa Bwana; Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza. Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.
    Mithali 11:1, 3
  • Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya; Bali mwenye haki atatoka katika taabu. Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila.
    Mithali 12:13, 17
  • Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.
    Mithali 28:13
  • Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
    Yakobo 5:16
  • lakini tumekataa mambo ya aibu yaliyositirika, wala hatuenendi kwa hila, wala kulichanganya neno la Mungu na uongo; bali kwa kuidhihirisha iliyo kweli twajionyesha kuwa na haki, dhamiri za watu zikitushuhudia mbele za Mungu.
    2 Wakorintho 4:2