Uaminifu
- Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake; 
Wakolosai 3:9 - 
Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote. 
Warumi 12:17 - 
tukitangulia kufikiri yaliyo mema, si mbele za Bwana tu, ila na mbele ya wanadamu. 
2 Wakorintho 8:21 - 
Mizani ya hadaa ni chukizo kwa Bwana; Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.  Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza. 
Mithali 11:1, 3 - 
Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya; Bali mwenye haki atatoka katika taabu. Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila. 
Mithali 12:13, 17 - 
Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema. 
Mithali 28:13 - 
Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii. 
Yakobo 5:16 - 
lakini tumekataa mambo ya aibu yaliyositirika, wala hatuenendi kwa hila, wala kulichanganya neno la Mungu na uongo; bali kwa kuidhihirisha iliyo kweli twajionyesha kuwa na haki, dhamiri za watu zikitushuhudia mbele za Mungu. 
2 Wakorintho 4:2